
mwili wa muasisi wa kundi la Tip Top Connection Abdu Bonge
Shughuli hiyo imefanyika nyumbani kwa marehemu Magomeni Kagera na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa waombolezaji ambao wameguswa kwa namna moja au nyingine kutokana na kifo hicho cha Marehemu Abdu Bonge.
Marehemu Abdu Bonge amepoteza maisha usiku wa juzi baada ya kusukumwa na kuanguka alipokuwa akiamua ugomvi wa majirani zake, na eNewz tunaiombea roho ya marehemu mapumziko mema mahala pema peponi, Aamin.
