Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Makorokocho waibuka mabingwa Dance100% 2016

Saturday , 24th Sep , 2016

Shindano la Dance100% 2016 limemalizika leo katika viwanja vya Don Bosco Jijini Dar es Salaam ambapo kundi la Makorokocho limeibuka na ubingwa na kujipatia kitita cha milioni 7, Kombe la Dance100% pamoja na cheti maalum.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kutoka Vodacom Jacquiline Materu akikabidhi mfano wa hundi ya milioni 7 kwa kusni la Timu Makorokocho

Ushindi wa Team Makorokocho umekuja baada ya makundi yote 6 kucheza raundi ambapo raundi ya kwanza Mega Mix waliyoandaliwa, na ilichezwa na makundi yote ikiwa na jumla ya alama 60% huku raundi ya pili ikiwa na alama 40% ambapo kila kundi lilijichagulia wimbo wake wa kucheza. .

Baada ya kazi ya raundi zote mbili kazi ya majaji ilikamilishwa na shughuli ya kumuisha matokeo na hatimaye kundi la Team Makorokochokuibuka na ushindi mwaka huu kutokana na uwezo waliouonesha katika raundi zote mbili na kuyapiku makundi yote.

Akizungumza baada ya kuibuka washindi wa shindano hilo Hamadi Abasi amesema umoja na mshikamano katika kundi lao ndicho chanzo kikuu cha wao kuweza kuibuka na ushindi wa shindano hilo.

“Sisi kutokana na umoja wetu tumekuwa zaidi ya ndugu ndiyo maana tumeweza kuwa wamoja katika mazoezi na kujituma na kuangalia wenzetu wana upungufu gani tukaufanyia kazi na hatimaye tukatangazwa washindi” Amesema Hamadi.

Hamadi ameongeza kuwa ushindi wao hauna ubishi wowote kwa kuwa ukiondoa majaji pia hadhira ambayo imeshiriki kutizama shindano wameona kazi ambayo wameoinesha .

Matokeo yote kwa makundi yote 6 yaliyoshiriki fainali ni kama ifuatavyo kwa mpangilio wa namba.

Timu Makorokocho
J Combat
D.D.I Crew
Clever Boys
Wazawa Crew na kundi la mwisho ni B.B.K Boys

Baadhi ya mashabiki ambao wameongea na EATV wamesema kundi hilo linastahili ushindi huo kutokana na namna ambavyo kuanzia mwanzo wa shindano hilo wameonesha dhamira ya kutaka ushindi kwa kuwa wabunifu kila siku wanaposhiriki shindano.

Shindano la Dance100% ambalo limefikia tamati leo litaoneshwa na EATV siku ya Jumapili saa moja jioni chini ya udhamini wa Vodacom pamoja na Coca – Cola.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ