Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Millen aliathirika kitabia" - Sophia Byanaku

Wednesday , 26th Jul , 2017

Baada Miss Tanzania 2001 Millen Magese  kupata mtoto wa kiume Julai 13 mwaka huu, rafiki wa karibu wa mrembo huyo anayejulikana kwa jina la Sophia Byanaku ameanika siri na tabia zilizokuwa zikisababishwa na ugonjwa uliomtesa zaidi ya miaka 20.

Millen Happiness Magese wakati akiwa mjamzito

Sophia ambaye aliwahi kuwa Miss Tanga 2001  amezungumza na  Nirvana ya EATV na kusema  kuwa Millen ameathirika kitabia na hali aliyokuwa nayo hata kumpelekea kuwa mtu mwenye hasira za mara kwa mara pasipo sababu.

"Matendo yake ya kuishi na watu yalikuwa yameathirika pia alikuwa mtu ambaye yupo 'So emotional. Kuna wakati alikuwa mtu mwenye hasira tu na ilihitaji watu wakaribu na  wanaofahamu ni kitu gani anapitia kuwa karibu naye ili kumfariji. Aliteseka sana lakini safari ambayo aliipambania imekuwa na matunda. ," alisema Sophia.

Bi Sophia Byanaku (Rafiki wa Millen Magese)

Bi. Byanaku ameongeza kuwa "Nimekuwa nikimshuhudia Millen akipata mateso haya tangu tukiwa watoto mpaka tunakuwa wakubwa. Furaha aliyo nayo kwa sasa imesababishwa na kutokuta tamaa kwake naimani atakuwa mama bora sana kwa mwanae Kairo. Lakini natamani kumuona akiendelea na kazi ya uanamitindo huku pia akiwa mama kwani naamini vyote anaweza kuvifanya kwa ubora zaidi.

Kwa upande wa kitaalamu Dokta wa maswala ya kina mama kutoka Dar es Salaam Dkt. Josephine Otieno amedai kitendo cha mtu aliyekuwa akisumbuliwa na hali ya 'Endometriosis' ni wazi atakuwa ametumia njia ya kitaalamu ijulikanayo kama 'In Vintro Fertilization' (Kupandikiza)"

'Kitaalamu kuna njia za kupandikiza kwa sababu kwa njia ya kawaida mtu mwenye matatizo ya 'Endometriosis' haiwezekani akapata mtoto. Njia ya IVF kwa hapa nyumbani inapatikana kwa gharama ya milioni 10 ambapo ni mara chache hutoa matokeo chanya kwa mara moja kwani wapo wanaopandikiza hata zaidi ya mara tatu mpaka nne"  alisema Dkt Otieno akizungumza na Nirvana.

Hata hivyo Millen aliwahi kukiri kwenye vyombo vya habari tofauti tofauti baada ya kuwa anabeba mimba kisha kutoka atafanya njia mbadala ya kuweza kufanikisha kupata mtoto.

HABARI ZAIDI

Bw. Nazar Nicholas (katikati) akikabiziwa tuzo ya WSIS 2024

Tanzania yashinda Tuzo WSIS 2024, nchini Uswisi

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton