Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Msimuhusishe mama Steve- Barnaba

Wednesday , 15th Aug , 2018

Mwalimu na mwanamuziki wa bongo Fleva, Barnaba Elias 'Barnaba Classic' amedai sio kweli wimbo wake mpya wa 'tuachane mdogo mdogo', ulikuwa unamlenga aliyekuwa mpenzi wake na mzazi mwenzake Zuu Namela bali anachokifahamu yeye kuwa amewaimbia watanzania waliompa dhamana ya kuimba.

Msanii Barnaba akiwa katika picha ya pamoja na aliyekuwa mpenzi wake Zuu Namela.

Barnaba amebainisha hayo leo Agosti 15, 2018 wakati alipokuwa anazungumza na www.eatv.tv ikiwa imepita siku chache tokea alipoachia wimbo wake huo, ambao tungo zake zimeonekana kwa namna moja ama nyingine zikimlenga mama Steve na kuibua mjadala mzito kwa mashabiki zake, kuwa akili yake bado ina muwaza mpenzi wake huyo licha ya kuwa wameachana muda.

"Siwezi kuzungumzia masuala ya mzazi mwenzangu. Mmeshawahi kuona wapi mtu anamuimbia wimbo mtu mmoja kila siku, mimi nawaimbia watanzania. Watu walianza kumjua Barnaba kabla ya kuingia kwenye mahusiano. Sijaanza kuimba mapenzi leo, nafanya kazi kwaajili ya watanzania ambao wamenipa dhamana ya mimi kuwepo hapa nilipo", amesema Barnaba.

Mbali na hilo, pia Barnaba amesema yupo mbioni kuachia albamu yake tatu aliyoipa jina la 'gold' huku akiwarusha dongo wasanii wenzake, waliokuwa wanalalamika kwamba albamu hailipi na kudai wao wenyewe ndio walikosea kwa kutoa albamu nyepesi nyepesi.

"Albamu yangu ya gold itaingia sokoni rasmi tarehe 31 mwezi huu na itakuwa na jumla ya nyimbo 25 kati ya hizo, tano zimeshasikika hewani. Nimeamua kuja na albamu kwasasabu ninaamini watanzania wanapenda na kuhitaji muziki mzuri. Hatuwezi kuliacha soko la albamu kwa kuhofia kuibiwa, wizi upo duniani kote", amesisitiza Barnaba.

Albamu hiyo kwa mara ya kwanza ilipangwa kutoka mwezi Februari 2018 lakini ikahairishwa hadi Juli 2018, kutokana na kile kilichoelezwa na Barnaba kuwa wadhamini wake wakuu watatu, walipendelea hivyo ambapo pia haikufanyika na badala yake kutoka rasmi Agosti 31 mwaka huu.

Gold itakuwa albamu ya tatu kwa Barnaba ambapo ya kwanza alitoa kwenye miaka ya 2009 kuelekea 2019 iliyojulikana kwa jina la njia panda na albamu yake ya pili aliiachia mnamo mwaka 2011 kuelekea 2012 iliyoitwa kisa changu.
 

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi