Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nay wa Mitego akumbana na rungu la BASATA

Monday , 27th Mar , 2017

Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limeufungia rasmi wimbo wa msanii Nay wa Mitego unaojulikana kwa jina la 'Wapo' kutumika kwa namna yoyote ile kuanzia leo kutokana na kutokidhi vigezo na masharti yaliyowekwa na baraza hilo.

Katibu Mkuu wa Baraza hilo Bwana Geofrey Mngereza (kushoto) na Msanii Nay wa Mitego

Katibu Mtendaji wa baraza hilo Bwana Geofrey Mngereza ametoa tamko hilo wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam na kutoa wito kwa wananchi na wadau kuacha kutumia kazi zilizopigwa marufuku kwani wakibainika hatua kali dhidi yao itachukuliwa.

“Kwa wale ambao watabainika wanatumia kazi hizi zilizopigwa marufuku ikiwa katika radio stesheni, bodaboda, mtaani hata katika ‘club’ hatua kali zitachukuliwa  dhidi yao kwa sababu wanaendelea kutumia vitu ambavyo vimefungiwa na baraza”. Alisema Godfrey

Pamoja na hayo Katibu huyo amefuta ile kauli yake aliyosema kuwa Nay wa Mitego na Prof Jay ndiyo wanaongoza kupeleka kazi zao kukaguliwa kabla ya kutoa na kusema alikuwa anawatolea mfano tu na laiti ingekuwa hivyo basi  msanii huyo angeshauriwa mapema kuwa wimbo huo haufai kutolewa kwa kukosa vigezo.

Aidha Katibu huyo amesema watamwita Nay wa Mitego ili kumpa nafasi ya kumsikiliza kwa upande wake ili aweze kusema ni kwanini ametoa wimbo wa aina hiyo.

Kwa upande mwingine Mngereza amesema wao na Jeshi la Polisi hawana uhusiano wowote kwa kuwa kila mtu anaongozwa na sheria zake alizokuwa nazo hivyo hata kukamatwa kwa msanii huyo amekamatwa kwa mujibu wa sheria za polisi na siyo BASATA.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ