Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Unataka kuondokana na madeni?, jifunze hapa

Thursday , 4th Oct , 2018

Madeni ni jambo ambalo linawaumiza sana watu wengi, lakini sababu kubwa inayopelekea watu kuwa na madeni ni kuwa na matumizi matumizi makubwa kuliko kipato halisi.

Mtu aliyeelemewa na madeni kwa kiasi kikubwa hawezi kufanya shughuli zake za kimaendeleo na uzalishaji mali kwa uhuru kwasababu pesa ambazo anazizalisha huishia mikononi mwa wadai wake. Fahamu njia hizi kubwa tano zitakazokusaidia  kuepuka au kupunguza kiwango chako cha madeni.

Tengeneza vyanzo vingi vya mapato

Tatizo la watu wengi sana ni kutegemea chanzo kimoja cha mapato, mfano mtu anategemea ajira pekee katika kuendesha mipango ya maisha yake kiasi kwamba hata kukitokea na dharura ya kuchelewa kwa mshahara, basi mtu huyo atalazimika kukopa. Jijengee vyanzo vingi vya mapato ili kuweza kumudu katika changamoto kama hizo.

Anzisha benki yako

Wahenga waliosema 'Akiba haiozi' hawakukosea, kwani suala la kujitunzia akiba sio tuu humfanya mtu kujiamini anapokumbwa na matatizo ya kifedha bali hata kukusaidia katika kutengeneza mtaji wako ambao utakuwezesha kuanzisha vyanzo vingi vya mapato vitakavyokuingizia pesa.

Pasipo na ulazima 'acha'

Usiingie katika madeni kwa vitu ambavyo havina ulazima katika maisha yako. Mkurugenzi mmoja wa shirikisho la mabenki nchini Singapore, Ong-ang Ai Boon akiwahi kusema kuwa " Ni muhimu kwa wateja kukopa pale tu panapokuwa na ulazima wa kufanya hivyo ", hiyo itakusaidia kwa kiasi kikubwa kukimbia madeni.

Jibane

Kujibana katika hili inamaanisha kwamba mtu anatakiwa ajifunze kutumia kidogo kwenye kile anachokipata. Matumizi yasizidi maingizo yako, kwasababu endapo utaruhusu matumizi kuwa makubwa kuliko unachoingiza tambua baada ya muda mfupi utaanza kukimbizana na wadai wako.

Usidanganywe

Kila mtu ana marafiki wengi katika maisha, wanaweza kuwa ni marafiki wazuri au wabaya. Kutokana na hilo mtu anapaswa awe makini na marafiki anaopenda kutembea nao hasa katika matumizi, mfano katika mitoko mbalimbali, wapo marafiki wanaopenda kutumia sana pesa katika starehe. Mtu unatakiwa kuwa na msimamo katika vitu kama hivyo ili kufikia malengo yako.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala