
Mratibu wa mbio hizo Hidaya Kamanga kutoka Mzizima Motor Sports Club, amesema mbio hizo zitaanzia katikati ya jiji na kupitia barabara za Ally Hassan Mwinyi, Bagamoyo, na kumalizikia Magereza Bagamoyo siku ya jumapili.
Sherehe rasmi ya kukabidhi zawadi na vikombe kwa washindi itafanyika Bagamoyo, Mei 22 mwaka huu.