Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Meck Sadick atoa neno baada ya Tarimba kukaa kando

Tuesday , 10th Jul , 2018

Makamu Mwenyekiti wa kamati ya kuivusha Yanga, Meck Sadick, amesema hana taarifa rasmi za kujiuzulu kwa Mwenyekiti wake katika kamati hiyo Tarimba Abbas, bali amezisikia tu kama watu wengine.

Tarimba Abbas (kushoto) na Meck Sadick (Kulia)

Sadick ambaye ni moja ya wanachama wenye heshima ndani ya klabu hiyo, ameeleza kusikitishwa na taarifa hizo na kuahidi kumfuata Tarimba na kuongea naye binafsi ili kujua nini sababu ya yeye kukaa kando.

''Kwasasa sio wakati mzuri wa kujadili kila jambo hata kama kweli kuna wakati mgumu tunapitia, Tarimba anaweza kuwa amekasirishwa na kitu binafsi pengine nikiongea naye mimi anaweza kusema tatizo na akarudi kwenye nafasi yake ila kwasasa tusubiri kwanza'', - amesema.

Tarimba alitangaza kuachia nafasi yake jana jioni kwa kile alichoeleza kuwa ni kutokuwepo kwa maelewano kati ya viongozi wa sasa wa klabu na viongozi wa kamati maalum ya kuivusha Yanga katika kipindi cha mpito ambayo yeye alikuwa anaiongoza kama Mwenyekiti.

Meck Sadick ambaye ni mkuu wa mkoa mstaafu aliyehudumu katika mikoa ya Dar es salaam na Kilimanjaro kwa vipindi tofauti, aliteuliwa kuwa makamu mwenyekiti wa kamati hiyo kupitia mkutano mkuu wa klabu uliofanyika Mei 20 huku Tarimba Abbas yeye akiteuliwa kuwa Mwenyekiti.

Tarimba ameiongoza kamati hiyo kwa siku 50, lengo kuu ikiwa ni kusaidia timu kwenye maeneo kadhaa ikiwemo usajili na maandalizi ya uchaguzi kwaajili ya kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Mwenyekiti Yusuf Manji. Aidha kamati hiyo ilipata baraka za baraza la wadhamini la Yanga chini ya Mwenyekiti George Mkuchika ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala bora.
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma