Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Milioni 15 zamuokoa Hans Poppe

Tuesday , 16th Oct , 2018

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Klabu ya Simba, Zacharia Hans Poppe amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo, Oktoba 16, 2018 na kusomewa mashtaka mawili na baadaye kuachiwa huru kwa dhamana.

Hans Poppe kulia akiingia kwenye mahakama ya Kisutu.

Hans poppe ameunganishwa katika kesi ya kughushi nyaraka za klabu na utakatishaji wa fedha inayomkabili Rais wa klabu hiyo, Evans Aveva na Makamu wake, Godfrey Nyange maarufu kama Kaburu.

Wakili wa Serikali, Shadrack Kimaro amewasomea washtakiwa wote mashtaka 10 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Katika mashtaka hayo 10 yanayowakabili viongozi hao, Hans Poppe anakabiliwa na mashtaka mawili, shitaka moja ni la kuwasilisha nyaraka za uongo na shitaka lingine ni la kughushi nyaraka ambayo kwa mujibu wa sheria mtuhumiwa anapata dhamana.

Inadaiwa kati ya Machi 10 na Septemba 30, 2016, Aveva, Kaburu na Hans Poppe waliwasilisha nyaraka za uongo kuonyesha Simba imenunua nyasi bandia zenye thamani ya dola za Kimarekani 40,577 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 90 za Kitanzania.

Baada ya kusomewa mashtaka yao mahakama ilitoa masharti ya dhamana kwa Hans Poppe yaliyomtaka kuwa na wadhamini wawili watakaosaini bondi ya shilingi milioni 15 kila mmoja masharti ambayo ameyatimiza na kupewa dhamana.

Kwa upande wa Aveva na Kaburu wamerudishwa rumande kwasababu mashtaka dhidi yao hayana dhamana. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 19.
 

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari