Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanachama wa Yanga waitwa kumalizana na jengo

Tuesday , 18th Jun , 2019

Baada ya mapema leo viongozi wa Yanga kuoneshwa eneo la kujenga uwanja wao huko Kigamboni na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda, uongozi wa Yanga umewaita wanachama wake.

Jengo la Yanga

Kupitia taarifa iliyotolewa usiku huu, uongozi wa klabu ya Yanga umetoa wito rasmi kwa wadau na wapenzi wa klabu hiyo ambao wangependa kufanya ukarabati wa vyumba katika Jengo la Makao makuu ya klabu hiyo lililopo mitaa ya Twiga na Jangwani jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Yanga, Dkt. Mshindo Msolla, amesema Kamati ya utendaji iliyoketi mwishoni mwa wiki imebariki kuanza kwa zoezi hilo kupitia wadau wenye mapenzi mema na klabu hiyo, ili kuwawezesha wachezaji kuishi katika jengi hilo. 

“Kwenye hafla ya Kubwa Kuliko nililieleza hili, nashukuru Kamati ya Utendaji imelipitisha, sasa rasmi tunawaalika wadau, ikiwa ni mwanachama mmoja, Tawi la Yanga, Kundi la WhatsApp au hata kampuni kufika klabuni kuanzia Alhamisi, ambapo tutakuwa tumeanisha gharama za ukarabati wa kila chumba hivyo watachagua kulingana na uwezo wao,” amesema Dkt. Msolla.

Amesema kukarabatiwa kwa vyumba katika Jengo la Yanga, kutasaidia kuondoa gharama kubwa ambazo timu hiyo imekuwa ikizitumia kwenye hoteli wakati wa kambi za mazoezi ya kawaida hasa timu inapokuwa jijini Dar es Salaam. 

“Tutatoa nafasi kwa vyumba kupewa majina ya wadau waliofanya ukarabati, mfano kama ni tawi la Makao Makuu, basi Chumba kitaitwa Makao Makuu kama watapenda, hivyo hii ni nafasi nyingine wa wadau wetu kusaidia maendeleo ya klabu yao kwa kuiepusha na gharama zinazoweza kuepukika,” alisema.

Jengo la Yanga lina jumla ya vyumba 28 pamoja na maeneo mengine muhimu ikiwemo eneo la kufanyia mazoezi ya Ndani (gym) ambayo pia inahitaji ukarabati mkubwa pamoja na kuwekwa vifaa vya kisasa.
 

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari