Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga na mchezaji watupiana mpira suala la madai

Monday , 3rd Dec , 2018

Wakati klabu ya Yanga ikiwa Jijini Mbeya tayari kwa mchezo wa ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Tanzania Prisons leo, imeendelea kuwakosa wachezaji wake kadhaa akiwemo nahodha Kevin Yondani.

Kikosi cha Yanga

Yondani hajaichezea klabu yake ya Yanga tangu aliporejea kutoka katika kambi ya timu ya taifa 'Taifa Stars' mwezi uliopita, ambapo taarifa mbalimbali zinadai kuwa mchezaji huyo anadai stahiki zake, jambo ambalo klabu imelipinga.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa klabu hiyo, Hussein Nyika, amefananua kuwa Yondani amebaki Jijini Dar es Salaam kumaliza matatizo yake binafsi ambayo yanamkabili hivyo hatocheza mechi ya leo.

Nyika amesema beki huyo mkongwe si kweli kuwa anaidai klabu bali ni mambo mengine yaliyosababisha ashindwe kusafiri na kikosi kuelekea Mbeya kwa ajili ya kipute hicho cha ligi.

"Ni kweli Yondani hajasafiri na timu, yupo Dar es Salaam kutokana na baadhi ya matatizo yanayomkabili na kuhusu kuidai Yanga si la kweli, ni mambo mengine tu yamesababisha asisafiri na timu," amesema.

Hivi karibuni Yondani aliwahi kukaririwa akisema kuwa ni kweli anaidai klabu yake lakini hiyo si sababu ya yeye kutoonekana uwanjani, akisisitiza kuwa atarudi kuitumikia klabu yake mambo yakikaa sawa.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP