Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga yaacha saba safari ya Majimaji

Sunday , 15th Jan , 2017

Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya soka Tanzania bara Yanga SC wanaondoka leo kwenda Songea tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu siku ya Jumanne katika dimba la Majimaji Songea huku ikiacha wachezaji 7 kwa sababu tofauti.

Donald Ngoma

Mshambuliaji hatari wa timu hiyo Mzimbabwe Donald Ngoma na Wazambia Justin Zulu na Obrey Chirwa ni kati ya wachezaji saba ambao hawatakuwamo safarini.

Kaimu katibu mkuu wa Yanga, Baraka Deusdedit amesema kwamba watatu hao wote bado ni majeruhi na wanaendelea na matibabu.

Baraka amesema kwamba winga Emmanuel Martin yeye hatakuwamo safarini kwa sababu yuko kwenye msiba wa mdogo wake  jijini Tanga, huku Vincent Bossou yupo na timu yake ya taifa, Togo kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) nchini Gabon, wakati mshambuliaji Malimi Busungu anaachwa kwa sababu hayupo fiti. 

Kwa mujibu wa Baraka benchi la ufundi la timu hiyo chini ya kocha Mzambia, George Lwandamina linataraji kuondoka na kikosi cha wachezaji 20 tu kwenye mchezo huo kikiongozwa na makipa; Deo Munishi ‘Dida’ na Benno Kakolanya, mabeki Hassan Kessy, Juma Abdul, Mwinyi Mngwali, Oscar Joshua, Andrew Vincent ‘Dante’, Pato Ngonyani, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kevin Yondan.

Viungo ni Said Juma ‘Makapu’, Thabani Kamusoko, Haruna Niyonzima, Juma Mahadhi, Deus Kaseke, Simon Msuva, Yussuf Mhilu, Geoffrey Mwashiuya na washambuliaji Amissi Tambwe na Matheo Anthony. 

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi