Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Zlatan aipa ubingwa Man United kwa masharti

Sunday , 15th Jan , 2017

Wakati United  ikijianda kuivaa Liverpool leo saa moja jioni, mshambuliaji wake mwenye maajabu Ibra Magic raia wa Sweden Zlatan Ibrahimovic amesisitiza kuwa Manchester United bado inaweza kutwaa ubingwa Ligi Kuu Uingereza msimu huu.

Zlatan Ibrahimovic

 

Man United imehaha kuendeleza kiwango bora katika hatua za awali msimu huu, lakini mashetani hao wekundu wameshinda mechi tisa mfululizo katika michuano yote, sita zikiwa ni Ligi Kuu.

Kikosi hicho cha Jose Mourinho bado kipo katika nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi lakini wamepunguza pengo la pointi dhidi ya vinara Chelsea hadi kufika pointi 10 na Ibrahimovic anaamini timu yake inaweza kupambana kutwaa ubingwa wa ligi iwapo wataifunga Liverpool katika uwanja wa Old Trafford siku ya leo.

"Ligi haitabiriki. Hakuna timu ambayo unaweza kusema itashinda na ikafanya hivyo," Ibrahimovic alikiambia Sky Sports News. "Chelsea imekuwa ikifanya vizuri, wanacheza mara moja kwa wiki, wana hali nzuri na nguvu nyingi kila wanapocheza, lakini walikuwa na wakati mgumu mwanzoni lakini walizinduka.

"Kama tutapanda pale na kuwasumbua, kila timu ina kipindi chake cha mafanikio. tumekuwa na wakati mzuri, tukishinda, tukipoteza na sasa tunashinda tena. Natumai tutaendelea hivyo na tunasubiri wengine wafanye makosa.

"Jumapili ni fursa nyingine ya kuchukua pointi kutoka nne bora. Kama tunaweza kuanza vita dhidi ya timu zilizo kwenye nne bora, baada ya kupoteza pointi nyingi ambazo hatukupaswa kuzikosa. Pengo limekuwa dogo sasa, na pointi hizo tunaweza kuanza kuzichukua kwa Liverpool,"

Ibrahimovic ambaye alitua Old Trafford kwa uhamisho huru amefunga magoli 18 katika michuano yote akiwa United, ikiwa ni pamoja na magoli 13 ya ligi

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala