Wednesday , 11th May , 2016

Mabingwa wa Ligi Kuu ya Soka nchini Uingereza, Leicester City wanataraji kufanya mazungumzo na kocha wao Claudio Ranieri kuhusu mkataba mpya mwishoni mwa msimu huu.

Muitaliano huyo ameweza kuwapa Mbweha hao taji la kwanza katika Historia ya klabu hiyo, tangu aliposaini mkataba wa miaka 3 mwaka uliopita.

Mabingwa hao mbali na kuanza mchakato wa mkataba mpya na kocha huyo, pia wapo katika kuhakikisha inawafunga mikataba mipya wachezaji muhimu wa klabu hiyo.