
Abdul Kambaya, ambaye pia ni miongoni mwa wanachama wa CUF waliosimamishwa
Kambaya ameyasema hayo katika kipindi cha East Africa Break Fast na kusisitiza kwamba mgogoro huo utaisha kwa pande zote kukaa chini na kujadili mustakabali wa chama chao na siyo watu wengine kuwaingilia kufanya maamuzi.
“Tutafanikiwa kuvuka mgogoro huu kama tutakaa chini kwa pamoja, tuzungumze na kuelewana lakini kama watu wengine wakiingilia na upande mmoja ukawaamini hatutafikia mwisho na wanachama watazidi kugawanyika” Amesema Kambaya
Mgogoro wa CUF umezidi kushika kasi baada ya Baraza Kuu la chama hicho lililoketi Zanzibar kutangaza kumvua uanachama Prof. Ibrahim Lipumba kwa ukiukaji wa katiba ya chama hicho huku Ofisi ya Msajili wa Vyama Vya Siasa ikitangaza kumtambua Prof. Lipumba kama Mwenyekiti halali wa chama hicho.