
Bondia Ibrahim Class
Muandaaji wa pambano hilo Jay Msangi amesema mpambano huo utatanguliwa na pambano kati ya Mtanzania Dullah Mbabe akipambana na Chengbo Zheng kutoka China katika uzito wa kilo 81 huku akiongeza kuwa mapambano hayo ambayo ni makubwa ya kimataifa yatasaidia mabondia hao kuwa katika maandalizi mazuri na ya mapema kwa ajili ya kuelekea katika mashindano ya Olimpiki ya mwaka 2020.
Msangi amesema, kwa sasa wanahitaji kuwa na maandalizi ya mapema kwa mabondia kwa ajili ya kuwawezesha kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali hususani yaliyo mbele yao kwa sasa ya Olimpiki.