Saturday , 3rd Jun , 2017

Wachezaji 31 wa timu ya Taifa ya Wanawake 'Twiga Stars' wataingia kambini Juni 7, kwa ajili ya kujiaandaa na michezo miwili ya kirafiki dhidi ya timu za wanawake za Dubai na nyingine kutoka nchini Kenya.

Kocha wa Twiga Stars, Sebastaian Nkoma akizungumza na waandishi

Kocha Mkuu wa timu hiyo, Sebastian Nkoma amesema wachezaji 10 kati ya hao wametoka katika Ligi Kuu ya soka ya Wanawake iliyomalizika mapema mwaka huu.

“Nitakuwa na kambi ya siku 12, baadaye nitacheza mchezo mmoja au miwili ya kirafiki Arusha na timu hii naiandaa kwa ajili ya fainali za Afrika (AFCON) zitakazofanyika Ghana mwakani,” amesema.