Thursday , 29th Nov , 2018

Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka nchini England Manchester City, wanashuka dimbani kuwakaribisha AFC Bournemouth Jumamosi hii, mechi ambayo itarushwa 'LIVE' kupitia EATV na TV 1.

Wachezaji wa Man City kushoto na AFC Bournemouth

Kuelekea mchezo huo, zifuatazo ni rekodi za timu hizo mbili ambapo Bournemouth ilipopanda ligi kuu msimu wa 2015/16 ina rekodi mbaya mbele ya mabingwa hao mara 5 wa EPL.

Katika msimu wao wa kwanza kwenye EPL, Bournemouth ilipoteza mechi zote mbili za nyumbani na ugenini. Msimu wa 2015/16 mechi ya kwanza ilichezwa Oktoba 17, 2015 ambapo Man City ilishinda 5-1 nyumbani na mechi ya pili ikapigwa April 2, 2016 ambapo Man City pia ikashinda 4-0 ugenini.

Msimu wa 2016/17, mechi ya kwanza ilichezwa Septemba 17, 2016 na Man City kushinda kwa mabao 4-0 kabla ya mechi ya pili kupigwa Februari 13, 2017 ambapo Bournemouth ilipoteza ikiwa nyumbani kwa mabao 2-0.

Msimu uliopita wa 2017/18 mchezo wa kwanza ulipigwa Agosti 26, 2017 , Bournemouth ikiwa nyumbani ilipoteza 2-1 kisha ikasafiri kwenda Etihad mwezi Desemba 23, 2017 na kupoteza kwa mabao 4-0.

Mechi ya kwanza msimu huu wa 2018/19 inachezwa Jumamosi hii kwenye dimba la Etihad. Je AFC Bournemouth itaondoa uteja kwa Man City? Usikose kutazama 'LIVE' kuanzia saa 11:30 jioni kupitia EATV na TV1.