Friday , 15th Aug , 2014

Mtayarishaji video mahiri, Abbas Adam pamoja na timu nzima inayomsimamia msanii Wabibi, wametangaza ziara kubwa Afrika Mashariki yenye lengo la kumtangaza msanii huyu na pia kufanya kolabo kadhaa na wasanii kutoka nje ya mipaka ya Bongo.

mtayarishaji wa video nchini Abas Adam

Abbas ameiambia eNewz kuwa, mpango huu utaanza na nchini Kenya ambapo watafanya video ya msanii huyu sambamba na kufanya kazi na wasanii wakubwa kama vile P Unit na wengineo.

Abbas ameelezea pia kuwa watasafiri pia kuelekea jijini Kampala nchini Uganda katika kutafuta soko zaidi kuitangaza kazi mpya ambayo imebatizwa jina 'Kitenge' itakayofanyiwa kazi pia nchini Afrika Kusini.