Mashabuki wa Simba na Yanga
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Yanga imetambulisha wimbo wake rasmi utakaotumiwa katika michuano mbalimbali kuanzia msimu huu, na kusisitiza kuwa ni wajibu wa wanachama na mashabiki kuufahamu wimbo huo.
Wimbo huo wa Yanga utaanza kutumika katika mchezo wao wa Kimataifa wa 'Wiki ya Wananchi', Agosti 4 dhidi ya Kariobangi Sharks ya Kenya.
Mahasimu wao Simba waliahidi kutoa wimbo wao rasmi wa klabu ifikapo Agosti 3, 2019, wimbo ambao utaanza kutumika katika mchezo wao wa Kimataifa wa Simba Day, Agosti 6 dhidi ya Power Dynamo ya Zambia.