Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mgawanyo wa zawadi katika Sprite Bball Kings 2019

Wednesday , 14th Aug , 2019

Mashindano ya tatu ya Sprite Bball Kings 2019 yanayoandaliwa na East Africa TV na East Africa Radio kwa kushirikiana na kinywaji cha Sprite, yanatarajia kuzinduliwa Jumamosi hii, Agosti 17 katika viwanja vya Mlimani City, Dar es Salaam.

Msimamizi wa Sprite Bball Kings 2019, Bhoke Egina

Maandalizi yamekamilika kwa asilimia kubwa kuelekea uzinduzi wake, ambapo siku ya uzinduzi itaambatana na usajili wa timu shiriki pamoja na burudani kadhaa kwa wageni ambao watahudhuria.

Akizungumza na waandishi wa habari leo katika ofisi za EATV, Msimamizi wa Sprite Bball Kings 2019, Bhoke Egina amesema kuwa wanatarajia ushindani mkubwa kutoka kwa washiriki huku akitaja zawadi ambazo zitatolewa kwa mabingwa.

"Mshindano yanatarajia kuanza siku ya Jumamosi, Agosti 17 pale Mlimani City ambapo tutaanza na usajili na tunaita timu zote kuja kujisajili kwa ajili ya kushiriki mashindano hayo. Huu ni mwaka wa tatu EATV na EA Radio inaendesha mashindano haya kwa lengo la kuukuza huu mchezo kwa Watanzania kutokana na kwamba haupewi kipaumbele", amesema Bhoke.

"Timu ambayo itashinda ubingwa itapata kiasi cha shilingi millioni 10, mshindi wa pili atapata milioni tatu na MVP atapata Sh milioni 2 pamoja na vikombe vitakavyotolewa kwa washindi wote", ameongeza.

Aidha Msimamizi wa mashindano amesema kuwa vigezo vitakavyozingatiwa ni pamoja na umri wa washiriki ambao ni kuanzia miaka 16, timu shiriki zinatakiwa kuwa na wachezaji wasiozidi 10.

Mashindano ya Sprite Bball Kings yalizinduliwa rasmi kwa mara ya kwanza Mei 3, 2017 na jumla ya timu 52 toka sehemu mbalimbali Tanzania zilijisajili.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa