
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa wa Hospitali hiyo Aminiel Aligaesha amesema waliofariki ni Asha Ally Seleman, na Avelina Pastory Aman.
Amesema kati ya majeruhi 11 waliobaki wanaoendelea kutibiwa hospitalini hapo, sita wapo wodi namba 22 ya Sewahaji na watano ICU.
Ajali hiyo ilitokea Agosti 10, 2019 mkoani Morogoro kwenye barabara ya Morogoro - DSM, baada ya lori la mafuta ya petroli kupinduka na kuwaka moto.