Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

'Nape alikuwa anatuma meseji usiku saa 8' - JPM

Tuesday , 10th Sep , 2019

Mbunge wa Mtama Mkoani Lindi Nape Nnauye, amemuomba msamaha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, hii ikiwa ni miezi kadhaa imepita tangu kusikika kwa sauti yake na viongozi wengine wa siasa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zenye maneno yasiyofaa.

Rais Magufuli (kulia) na Nape Nnauye (kushoto).

Mbunge Nape amekutana na Rais Magufuli leo Septemba 10, 2019, Ikulu ya Dar es Salam, ambapo mara baada ya mazungumzo yao amemshukuru Rais kwa kukubali kukutana naye na kumsamehe.

''Kwanza nimekuja kumuona kama Baba yangu, kwa sababu wote mnajua yametokea mambo mengi hapa katikati na mimi kama mtoto wa CCM, mimi kama mwanaye nilidhani ni vizuri nije niongee na Baba yangu na namshukuru kwamba alinipa fursa ya kumuona na ameniambia amenisamehe'' amesema Nape.

Kwa upande wake Rais Magufuli amesema, Nape amekuwa akiomba kukutana nae mara nyingi kupitia kwa watu mbalimbali wakiwemo wasaidizi wake, viongozi wastaafu na viongozi wa CCM na kwamba baada ya kukutana nae na kumuomba radhi ameamua kumsahehe.

''Kikubwa anachozungumza naomba Baba unisamehe,  kwahiyo inauma kusamehe kunaumiza lakini nasema kwa dhati nimemsamehe'', amesema Rais Magufuli.

Ikumbukwe kuwa Rais Magufuli amemsamehe Nape ikiwa ni siku chache tu, tangu alipotangaza kuwasamehe wabunge William Ngeleja na January Makamba.
 

Zaidi Tazama video hapo chini

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa