Sunday , 15th Sep , 2019

Jeshi la Polisi Kenya linawashikilia Watanzania 6 kwa tuhuma za kufanya shughuli za ombaomba eneo la Makueni, lilipo Mashariki mwa nchi hiyo.

Kamanda wa Polisi wa Makueni Joseph Ole Napeiyan, amesema Watanzania hao wamekuwa wakitumia viti vya watu wenye ulemavu, na kufanya shughuli zao za kuomba katikati ya Makueni.

Siku za hivi karibuni tulipokea malalamiko kutoka kwa  wakazi wa maeneo ya Migori wakilalamikia kuwepo kwa watanzania hao ambao wamekuwa wakifanya shughuli hizo za kuomba msaada kwa wakenya” Amesema RPC Makueni, Joseph Ole Napeiyan

Ameongeza kuwa kati ya hao Watanzania 6, mwanaume ni 1 na wanawake 5 huku mwanamke mmoja akiwa na mtoto, na kueleza jeshi hilo kuwashikilia kwa ajili ya uchunguzi.

Hivi karibuni uongozi wa Serikali eneo la Migori, uliomba Serikali ya Kenya kuwaondoa ombaomba wote wa Kitanzania waliopo nchini humo.