Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Jinsi daraja Tanga lilivyowakwamisha wananchi

Sunday , 13th Oct , 2019

Daraja la Mto Mnyuzi lililopo Kijiji cha Jitengeni, Kata ya Segera lililopo katikati ya mpaka wa Wilaya ya Korogwe na Handeni mkoani Tanga limekatika kufuatia mvua zilizonesha mfululizo na kusababisha kukatika kwa mawasiliano kati ya abiria wanaotoka Arusha kwenda Tanga na Arusha kwenda

Dar es salaam baada ya maji kujaa kupita kiasi katika barabara hiyo.

Mvua hizo pia zilisababisha vifo vya watu saba waliosombwa na maji yanayotokana na mafuriko ya mvua.

Tokea jana saa tano asubuhi magari kutoka Arusha kwenda Tanga na Arusha Dar es salaam, yamelazimika kupiga kambi katika eneo hilo wakisubiria msaada wa namna gani daraja hilo litaweza kujengwa ili kuruhusu mawasiliano.

EATV na EA Radio Digital ilifanikiwa kufika katika eneo hilo na kufanya mahojiano na abiria waliokwama kwenye eneo hilo ambapo walilalamika kuhusu gharama kuwa kubwa kutokana na chakula pamoja na huduma za kijamii kuwa juu kupita kiasi na kushindwa kumudu gharama hizo.

''Tunaomba serikali ifanye jitihada za makusudi za kusaidia eneo hili liweze kupitika tunapata adha kubwa sana kwani tokea jana saa tano asubuhi  tupo kwenye eneo hili na watoto wadogo vyakula hatuna na bei za hapa hatuzimudu,''amesema Amani Bakari ambaye ni mmoja wa abiria.

Kwa upande wao madereva waliokwama katika eneo hilo wameiomba serikali kuangalia namna ya kutatufa njia ya sahihi ya kukomesha tatizo hilo kwani siyo mara ya kwanza kujaa maji katika daraja hilo ambapo walisema hali hiyo inahatarisha sana maisha ya wananchi.

Wakazi wa kijiji hicho nao wameiomba serikali kutafuta njia ya kumuokoa mzee mmoja aliyepanda juu ya mti wa muembe kwajili ya kujiokoa tokea jana ambapo alipiga simu na kuomba msaada huo baada ya mafuriko kulikumba eneo alilokuwepo huku mifugo yake ikisombwa na maji.
 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja