Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Hata Mwalimu aliwachapa kina Sitta Ikulu"- Wasira

Monday , 14th Oct , 2019

Aliyewahi kuwa Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Stephen Wasira amezungumza jinsi kipindi cha miaka 7 ya Ukuu wa Mkoa wa Mara ulivyomsaidia kumfahamu vizuri hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Stephen Wasira

Wasira ameyabainisha hayo leo Oktoba 14, 2019, wakati wa Kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha Baba wa Taifa, lililofanyika Kijijini Butiama mkoani Mara.

''Kama kuna wakati nimejifunza juu ya maisha ya Mwalimu ni katika kipindi cha mika 7 na nusu ya Ukuu wa Mkoa wa Mara kwasababu alikuwa anakuja hapa kila Pasaka na Christmas, anakaa sana na kiserikali mimi ndiye nilikuwa mwenyeji wake, Mwalimu alikuwa anasikiliza sana hata kama unaongea vitu vya hovyo hovyo anakusikiliza na wala hakuambii ukae'', amesema Wasira.

Aidha Wasira amelizungumzia suala la Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila la kuwachapa Wanafunzi viboko akisema kuwa hata Mwalimu aliwahi kufanya hivyo kwa kina hayati Samuel Sitta walipokuwa wanafunzi wa Chuo Kikuu.

''Nchi inaendeshwa kwa utaratibu, kama utaratibu ni viboko wanachapwa tu, maana hata Mwalimu alishawahi kuwachapa kina Sitta viboko pale Ikulu, wakiwa Wanafunzi wa Chuo Kikuu, walijifanya vituko aliwachapa mwenyewe, aliuvua Urais akawa Mwalimu, inategemea hali ilivyo kwa wakati huo'', ameongeza.

Wasira ameendelea kumsifia Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, kwamba alikuwa ni mtu anayechukia umaskini na hakutaka huo utajiri awe nao peke yake na kwamba kama angetaka hivyo huenda ndiyo angekuwa ni tajiri mkubwa Afrika na Duniani.
 

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ