Whozu
Whozu amesema kwamba maisha yake hapendi kuyaweka sana mtandaoni kwahiyo hakuna haja ya kila mtu kujua anachokifanya lakini ukweli anao yeye na vitu anavyomiliki vina thamani kubwa.
"Simzuii mtu kuniongelea vibaya, ninaangalia maisha yangu. Hii cheni hapa ni kodi ya mtu kabisa tena ni ya miezi sita au mwaka mzima", amesema Whozu.
"Ninachoweza kusema ni kwamba watu waangalie na kusapoti kazi zangu tu kama mwanzo. Kuhusu hela zangu mimi sichezei, ninafanya vitu vya msingi", ameongeza.
Whozu anatamba na wimbo wa Doko huku pia akishirikishwa katika wimbo wa Sensema wa Hamisa Mobetto ambao umechiwa hivi karibuni.