Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TAKUKURU yatangaza kutaifisha mali za watu hawa

Tuesday , 26th Nov , 2019

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Brigedia Jenerali John Mbungo, amezitaka taasisi na mashirika yote yaliyotafuna fedha za vyama vya Msingi na Ushirika kuzirudisha haraka iwezekanavyo kuanzia leo Novemba 26, na kwamba wasipofanya hivyo watafikish

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Brigedia Jenerali John Mbungo, akikabidhiwa ripoti na Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga.

 

na kutaifishwa mali zao.

Hayo ameyabainisha wakati akipokea muhtasari wa uchambuzi wa ukaguzi wa Vyama vya Ushirika, uliofanywa na Shirika la Ukaguzi wa Vyama vya Ushirika (COASCO), kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Kilimo katika mji wa Serikali ulioko Mtumba Jijini Dodoma.

"Natoa rai kwa wale wote wana Ushirika, Bodi za Ushirika na wote waliokuwa wanakusanya fedha za Saccos, waanze kurudisha fedha hizo kuanzia leo, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao tutawachunguza na hatutaacha jiwe lolote ambalo halijageuzwa kwenye hilo suala la Ushirika" amesema Brig Jenerali Mbungo.

Aidha Jenerali Mbungo ameongeza kuwa "Ubadhirifu wowote haukubaliki kwani ni wizi kama wizi mwingine, endapo hawatarudisha sisi uchunguzi tutauanza mara moja pale ambapo kutakuwa na ushahidi hatua kali zitachukuliwa ikiwemo kupelekwa mahakamani, lakini hata kabla ya kushtakiwa kwa kushirikiana na Mwendesha Mashtaka wa Serikali tutapeleka maombi ya kutaifishwa mali walizonazo" ameongeza.

Kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019, Serikali ilitoa maagizo kwa Shirika la COASCO kukagua Vyama vya Ushirika vyote, ambapo hadi tarehe 30 Juni, 2019 Vyama vya Ushirika vilivyosajiliwa vilikuwa 11,410, kati ya Vyama hivyo, Vyama hai ni 6,463, Vyama Sinzia ni 2,844 na Vyama ambavyo havipatikani 2,103.

Kutokana na maagizo hayo, hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2019 COASCO ilikagua Vyama vya Ushirika vipatavyo 4,413 sawa na asilimia 102.63 ya lengo la Serikali la kukagua Vyama 4,300.

Katika vyama hivyo 4,413 vilivyokaguliwa, vyama 303 (6.87%) vilipata Hati inayoridhisha, vyama 2,378 (53.89%) vilipata Hati yenye shaka, vyama 879 (19.92%) vilipata Hati isiyoridhisha na vyama 853 (19.32%) vilipata Hati mbaya.

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi