Wednesday , 4th Dec , 2019

Mwanamke mmoja aliyetambulika kwa jina la Sharon Achieng (23) kutokea nchini Kenya, amekamatwa na polisi katika kituo cha Siaya  kwa kosa la kutaka kumuuza mwanaye wa kiume aliye na umri miaka mitano.

Gari la Polisi nchini Kenya

Mtuhumiwa huyo alikamatwa kutokea kijiji cha Anduro, ambapo alitaka kumuuza mwanaye kwa mwanamke aliyejulikana kwa jina la Irene, kwa shilingi milioni 2 za Kenya sawa na milioni 45 pesa ya kitanzania.

Joseph Aloo ambaye ni kiongozi msaidizi wa kituo hicho cha polisi amesema, wanamshikilia mtuhumiwa huyo kwa kujaribu kumuuza mwanaye kwa mtu ambaye anafanya kazi ya ulinzi.

Pia anajitetea kwa kusema alikuwa anashindwa kumlea mtoto huyo peke yake kwa kuwa mume wake amemkimbia.

Aidha kwa upande wa Irene ambaye alipelekewa mtoto huyo ili kumnunua ameeleza kuwa, Sharon Achieng alimleta mtoto huyo huku akisema yeye ni yatima na anaishi kwa bibi yake pia hajawahi kuolewa.