Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Maamuzi mapya ya BASATA kwa Rosa Ree

Saturday , 7th Dec , 2019

Baraza la Sanaa la Taifa "BASATA"  limempunguzia adhabu rapa wa kike nchini Tanzania Rosa Ree ya kumfingia miezi 6, na kumruhusu kuendelea na shughuli zake za kisanaa.

Picha ya msanii HipHop Rosa Ree

Barua hiyo  imetoka kwa Katibu Mtendaji wa baraza hilo Godfrey Mngereza  na imeandikwa,

"Baraza la sanaa la Taifa linapenda kukutaarifu kuwa ombi lako la kupunguziwa adhabu limekubaliwa baada ya kujutia kosa lako na kumuandikia barua Mh. Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo ili kuomba kupunguziwa adhabu", Barua kutoka Basata.

Aidha barua hiyo iliendelea kusema "1. Kuanzia tarehe ya barua hii, unaruhusiwa kuendelea na shughuli za sanaa, hivyo adhabu uliyopewa ya kufungiwa miezi 6  imeondolewa, 2. Kulipa faini ya milioni 2, kama ulivyoagizwa na hii ilipwe ndani ya mwezi mmoja".

Kupitia ukurasa wa mtandao wa Instagram Rosa Ree ameandika "Napenda kutoa shukrani kwa ofisi ya Waziri wa sanaa, habari, utamaduni na  michezo Mhe. Harrison Mwakyembe na BASATA, kwa kuniruhusu kuendelea kufanya shughuli zangu za sanaa, naahidi kufanya kazi zangu ipasavyo na kuendelea kuipeperusha bendera ya nchi yangu"

Ikumbukwe mwezi uliopita Basata walimfungia Rosa Ree kwa muda wa miezi sita na kumtaka alipe faini ya Milioni 2, kwa makosa mawili ambayo ni kuachia video iliyokosa maadili pamoja kufanya kazi nje ya nchi bila kuwa na kibali.
 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja