Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kibonge mwepesi aeleza sababu ya kupigwa na AJ

Tuesday , 10th Dec , 2019

Bondia Andy Ruiz Jr 'kibonge mwepesi' mwenye uraia wa Mexico na Marekani, amesema kuwa kuongezeka uzito pamoja na kula bata zaidi na marafiki zake, ndiyo sababu kubwa iliyopelekea yeye kuchezea kichapo mbele ya Bondia Anthony Joshua.

Bondia Andy Ruiz na Anthony Joshua wakiwa ulingoni.

Andy Ruiz amesema hayo alipodakwa na kamera za mtandao wa TMZ, wakati anashuka katika Airport ya jiji la Los Angeles Marekani, siku ya Desemba 9, 2019.

"Nahisi nilikuwa nakula kila kitu ndiyo maana nimeongezeka uzito, nilikula sana bata na kufurahia maisha na marafiki zangu pamoja na kunywa vinywaji vya Corona, kwa hili umbo itabidi nifanye mazoezi nchini Mexico na jijini California na nitalichukulia hili jambo kwa umakini zaidi" amesema Andy Ruiz.

Aidha amesema kwa sasa ana mpango wa kuweka kando mambo ya kula bata na marafiki zake, pia ametenga muda wa kukaa na familia yake huku akifanya mazoezi kwa ajili ya pambano la tatu na anataka kurudisha mikanda yake iliyoenda kwa Anthony Joshua.

Katika pambano lake la raundi ya pili alilopigana siku ya Desemba 7, 2019, Andy Ruiz alikuwa na kilo 284,na kwamba ameongezeka kilo 15 tofauti na zile za mwanzo, alipopigana na Anthony Joshua katika pambano lake la kwanza mwezi Juni, lililompatia ushindi wa KO katika raundi ya 7.
 

HABARI ZAIDI

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu