Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manara azitaka pointi 6 za Mwanza, Mbao FC wajibu

Wednesday , 15th Jan , 2020

Kuelekea mchezo wa Ligi kuu soka Tanzania Bara kesho Alhamis 16, 2020, klabu ya soka ya Mbao FC imesema imejiandaa vizuri licha ya wapinzani wao Simba kuwa na kila kitu kinachoweza kuwapa ushindi.

Kushoto ni Haji Manara na kulia ni wachezaji wa Mbao FC

Akiongea na EATV & EA Radio Digital, kocha msaidizi wa Mbao FC Abdulmutik Hajji ameweka wazi kuwa wamefanya maandalizi yao vizuri kwa kuzingatia ubora wa wapinzani wao.

'Tumejiandaa vizuri kuelekea mchezo wa ligi kuu kesho dhidi ya Simba lakini tunaiheshimu Simba kutokana na uzoefu mkubwa ilionao', amesema Hajji.

Kwa upande wa msemaji wa Simba Haji Manara amesema wanataka kupata pointi zote 6 za michezo miwili ya Mwanza ambayo ni dhidi ya Mbao FC na Alliance FC.

'Sasa akili yetu tuelekeze Mwanza katika mechi mbili ngumu zijazo, tushirikiane kupata pointi sita za CCM Kirumba, Insha'Allah tutafanikiwa', ameandika Manara.

Msimu huu Mbao FC wamecheza mechi 16 ambapo wameshinda mechi 4, Sare 6 na kufungwa mechi 6, wakati Simba wamecheza mechi 14, wameshinda 11, sare 2 na kufungwa 1.

Katika dirisha dogo la usajili Mbao FC wamesajili wachezaji watatu ambao Omary Wayne kutoka Ndanda SC walinzi Hussein Iddi kutoka Mtibwa Sugar na Mackyada Franco kutoka Coastal Union.

Simba wao wamesajili mchezaji mmoja ambaye ni Luis Miquissone kutoka UD Songo ya Msumbiji.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi