Eneo la Kanolo ambalo daraja limesombwa na maji
Hayo yamebainishwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani humo ilipotembelea mradi huo ikiongozwa na Katibu Tawala wa mkoa, Mhandisi Emmanuel Kalobelo kufuatia daraja lililopo eneo la Kanolo wilayani Kilombero kusombwa na maji usiku wa Januari 24 kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.
Mkuu wa Wilaya ya Kilombero na Wakala wa Barabara mkoani Morogoro wamesema hawaridhishwi na kasi ya ujenzi wa mradi huo kwani mpaka sasa mkandarasi yuko nyuma ya muda kwa asilimia 90.
Naye Mhandisi Mshauri katika mradi huo, Maburugi Mapambano amekiri kuwa mradi huo uko nyuma huku wananchi wakiiomba serikali iangalie uwezekano wa kubadilisha mkandarasi huyo.