Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Virusi vya Corona vinavyoathiri michezo duniani

Friday , 13th Mar , 2020

Dunia ipo katika tahadhari kubwa hivi sasa kufuatia mlipuko wa virusi vya Corona vilivyoanza mwanzoni mwa mwaka 2020 nchini China. 

Mchezo wa PSG dhidi ya Dortmund

Virusi hivyo vimeendelea kuiathiri dunia katika nyanja mbalimbali ikiwemo katika tasnia kubwa ya kimichezo, ambapo katika kipindi kifupi cha hivi karibuni, shughuli mbalimbali katika tasnia hiyo zimesimamishwa.

Katika mchezo wa mpira wa kikapu, Ligi ya Kikapu nchini Marekani NBA imesimamishwa kwa muda usiojulikana kuyokana na kuenea kwa kasi kwa virusi hivyo, huku michuano ya Formula 1 katika Australian GP ikisimamishwa baada ya mmoja wa wahusika katika timu ya McLaren kukutwa na virusi hivyo.

Shirikisho la Tennis duniani ATP, pia limethibitisha kusimamisha mashindano ya wanaume mpaka mwishoni mwa mwezi Aprili, ikenda sambamba na kusimamisha michuano hiyo katika miji ya Barcelona, Miami, Budapest, Houston na Marrakech.

Katika soka, ligi mbalimbali barani Ulaya na Amerika zimesimamishwa kwa muda ikiwemo, Ligi ya Uholanzi 'Eredivisie', ligi ya Italia 'Serie A', ligi ya Hispania 'LaLiga', ligi ya Marekani 'MLS', ligi ya Mabingwa barani Ulaya na baadhi ya michezo ya ligi ya Europa na ligi ya Uingereza 'PL'. 

Baadhi ya timu zimeathirika na virusi hivyo mpaka sasa, ambapo wachezaji wake pamoja na baadhi ya watu wa benchi la ufundi wamekutwa na virusi vivyo. Timu hizo ni Juventus, Leicester City, Arsenal, Chelsea, Manchester City na Real Madrid. Shirikisho la Soka barani Ulaya UEFA linakutana kujadili uwezekano wa kusogeza mbele michuano ya Euro na michuano ya vilabu barani Ulaya kufuatia tishio hilo.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa