Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Abdi Banda kuhusu kuhusishwa na virusi vya Corona

Wednesday , 18th Mar , 2020

Mlinzi wa klabu ya Highlands Park ya nchini Afrika Kusini na timu ya taifa ya Tanzania, Abdi Banda amezungumzia tetesi kuhusu kukumbwa na virusi vya Corona.

Abdi Banda

Banda ametoa taarifa hiyo baada ya tetesi mbalimbali kusambaa katika mitandao ya kijamii zikimuhusisha mlinzi kukumbwa na virusi vya Corona na kupelekea kutengwa na timu yake ili aweze kurejea katika hali yake ya kawaida.

Kupitia mtandao wa Instagram, Banda amekanusha taarifa kuhusu kukubwa na virusi vya Corona, ambapo amesema, "napenda kutoa shukrani zangu kwa wote mlioguswa/shtushwa na habari juu yangu, kikubwa kila kitu kimeenda sawa".

"Kwa baraka za Mwenyezi Mungu imegundulika haukuwa ugonjwa unaosumbua kwa sasa duniani (virusi vya Corona). Ahsanteni sana MUNGU awabariki", ameongeza.

Abdi Banda aliitwa katika kikosi cha timu ya taifa Taifa Stars, kilichokuwa kikijiandaa na mchezo wa kuwania kufuzu michuano ya AFCON dhidi ya Tunisia lakini hakuwasiri kambini, hali iliyozusha wasiwasi huo.

Hata hivyo mchezo huo uliahirishwa na Shirikisho la Soka barani Afrika CAF kutokana na tishio la kusambaa kwa virusi vya Corona.

HABARI ZAIDI

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji