Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Hatujazuiliwa kukutana, uchaguzi upo" - JPM

Thursday , 26th Mar , 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amesema kuwa vikao vya kawaida vya watendaji wa Serikali vitaendelea na hata Uchaguzi Mkuu utafanyika kama ilivyopangwa.

Rais Magufuli

Amesema hayo leo, Machi 26, 2020 katika hafla ya kupokea ripoti kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali CAG na ripoti ya TAKUKURU katika Ikulu ya Chamwino Jijini Dodoma.

Rais Magufuli amesema kuwa hata nchi ambazo zimeathirika zaidi na virusi vya Corona, bado mabunge na mabaraza yao yanaendelea na kusema kuwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu utafanyika.

"Hatujazuiliwa kukutana, leo nimesoma gazeti moja linasema 'Madiwani wafanya kikao cha Madiwani', sijui alifikiri vikao vya madiwani vimezuiliwa kwa sababu ya Corona?. Sisi tunaendelea kukutana katika mikutano hii ya kawaida na hata Bunge ndio maana linaendelea", amesema Rais Magufuli.

"Kazi lazima iendeleea kufanyika na uchaguzi tutafanya tu, wapo wengine wanafikiri nitaahirisha, ni nani anataka kukaa kwenye maofisi haya muda wote huu", ameongeza Rais Magufuli.

Katika ripoti ya ukaguzi iliyowasilishwa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG, Charles Kichere, jumla ya hati 1084 za Taasisi za Serikali Kuu, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Mashirika ya Umma, miradi ya maendeleo na Vyama vya Siasa kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2019 zimekaguliwa. Hati zinazoridhisha ni 1017, zenye shaka ni 46, hati zisizoridhisha ni 7 na hati mbaya 12. 

Pia Rais Magufuli amempandisha cheo aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brigedia Jenerali, John Mbungo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo kwa kazi nzuri aliyoifanya ikiwemo ya kurejesha bilioni 8.8 walizodhulumiwa wananchi.
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma