Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wizara yazungumzia watoto waliofunga ndoa

Thursday , 14th May , 2020

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Dkt Avemaria Semakafu amesema kuwa kwa yeyote aliyehusika ama kuhamasisha vitendo vya ubakaji na ngono kwa watoto wadogo, adhabu yake ni kifungo cha miaka 30 na kwamba lazima sheria itafuata mkondo wake.

Kushoto ni watoto wanaodaiwa kufunga ndoa mkoani Geita, na kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Dkt Avemaria Semakafu.

Dkt Avemaria ameyabainisha hayo leo Mei 14, 2020, wakati akizungumza na kipindi cha Supa Breakfast cha East Africa Radio, kinachoruka kila siku za Jumatatu hadi Ijumaa, kuanzia saa 12 Alfajiri hadi saa 4 Asubuhi.

"Mtu yeyote anayetembea na mwanafunzi wa Sekondari ama Msingi ni kitendo cha kubaka, kwahiyo kama kuna hilo tukio limetokea, mpaka linaripotiwa ina maana vyombo vya ulinzi na usalama vimeona, kwahiyo sheria zipo na nadhani ile miaka 15 na 30 inawahusu wahusika wote, hivyo siyo suala la Wizara ya Elimu ni suala ambalo lipo kisheria na misingi ambayo imepitishwa na Bunge" amesema Dkt Avemaria.

Aidha Dkt Avemaria akizungumzia suala la uwepo wa sheria ya kupima mimba watoto watakaporejea mashuleni amesema, "Hakuna sera wala waraka unaotuagiza kupima mimba wanafunzi watakaporejea shuleni, kama Wizara tunachoangalia kwa sasa ni kuandaa mazingira salama ya wanafunzi watakaporejea".

Hivi karibuni liliripotiwa tukio la aina yake, lilionesha watoto wa Darasa la Pili na la Nne wakiwa wamefunga ndoa huko mkoani Geita.
 

 

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari