Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TMDA yatoa kibali hiki kwa Precision Air

Thursday , 11th Jun , 2020

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imetoa idhini ya utambuzi ya miaka 3 kwa Shirika la ndege la Precision Air Tanzania Plc, inayotambua na kuruhusu uzalishaji wa Barakoa.

Moja ya ndege za Shirika la ndege la Precision Air

Hatua hiyo imekuja baada ya Precision Air kuwasilisha maombi kwa mamlaka hiyo na kufudhu ukaguzi uliofanywa ili kutathimini ubora na wa bidhaa (Barakoa) na mazingira ya kiwanda cha uzalishaji.

Akizungumzia mafanikio hayo, Mkurugenzi wa Precision Air Bw. Patrick Mwanri amesema shirika hilo litaanza uzalishaji wa  Barakoa kwa ajili ya wafanyakazi lakini pia wakitarajia kuziingiza sokoni kwa ajili ya kuuzwa kwa umma.

“Tunaishukuru TMDA kwa kutupatia kibali, kwani hatua hiyo itatuwezesha kuzalisha Barakoa zetu wenyewe tukiwa tunalenga kuwalinda wafanyakazi pamoja na abiria wetu. Tumezingatia muongozo wa Serekali kupitia wizara ya Afya na ile ya Utalii juu ya kufanya shughuli zetu huku tukiwalinda wafanyakazi na abiria wetu dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Corona.” Ameeleza Bw. Mwanri.

Bw.Mwanri amefafanua zaidi kuwa awamu ya kwanza ya uzalishaji wa Barakoa hizo utalenga kwanza wafanyakazi wa Precision Air na kwamba awamu ya pili itahusisha uzalishaji mkubwa kwa ajili ya kuziingiza sokoni kwa gharama nafuu ili kusaidia katika mapambano dhidi ya ugonywa wa korona.

Katika hatua nyingine,kuanzia tarehe 15 juni shirika la ndege la Precision Air linatarajia kurejesha safari zake za Zanzibar, Arusha  na Bukoba ambazo hapo awali zilipunguzwa kutokana na kushuka kwa abiria kulikosababishwa na hofu dhidi ya Corona.

Precision Air ni shirika la umma lililoanzishwa mnamo mwaka 1993 na linatoa huduma za usafiri  wa anga kwenda sehemu mbali mbali ndani na nje ya nchi. Safari zake huanzia makao yake makuu Dar es Salaam, kuelekea Arusha, Kilimanjaro, Serengeti, Mtwara, Kahama, Bukoba, Mwanza, Zanzibar, Tabora, Serengeti, Dodoma, Nairobi na Entebbe. (Safari za Nairobi na Entebbe zikiwa zimesitishwa kwa muda kutokana na makatazo yaliyotolewa na nchi husika kama njia za kuzuia kusambaa kwa maambukizi ya ugonjwa wa  Corona.) Huduma nyingine zinazotolewa na shirika la Precision Air ni pamoja na huduma za usafirishaji mizigo.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi