Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kinana asamehewa, Magufuli amtumia salamu Membe

Friday , 10th Jul , 2020

Chama cha Mapinduzi (CCM), kimemsamehe aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Abdulrahman Kinana, aliyekuwa amesimamishwa baada ya kupewa adhabu ya kalipio la miezi 18, baada ya kukiuka maadili ya chama na kusema kuwa kuanzia sasa anakaribishwa kuendelea kushiriki na wanachama wenzake.

Kushoto ni aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, katikati ni Rais Dkt Magufuli na kulia ni aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana.

Rai na msamaha huo umetolewa leo Julai 10, 2020, na Mwenyekiti wa chama hicho Dkt Magufuli, wakati chama hicho kikiendelea na Mkutano wa Halmashauri Kuu ya chama ikiwemo uchaguzi wa kupata jina la mgombea atakayepeperusha bendera ya chama hicho kwa ajili ya kugombea Urais wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Ndugu yetu huyu aliomba radhi hadharani ni kitendo kigumu sana kwa watu wa kawaida kukifanya, mimi alinigusa sana,nina uhakika hata ninyi Wajumbe iliwagusa sana, alikuwa amepewa adhabu ya kalipio la miezi 18, na hakukataa na mpaka sasa ametumikia miezi mitano sasa, niliona ndugu zangu niwaombe kama itawezekana tumsamehe" aliomba Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli akimzungumzia aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe amesema kuwa, "Yule mwingine ambaye sitaki kumtaja jina, yule ameshaondoka moja kwa moja adhabu ile si mmeikubali ya kumfukuza moja kwa moja?".
 

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari