
Upande wa kushoto ni Idris Sultan, kulia Steve Nyerere
Kupitia post aliyoweka kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter Idris Sultan ameandika kuwa, "Sitaki kuwa mnafki, kaka Steve juzi kaniongelea mbovu sana kwenye interview, mambo ambayo hata kama ni kweli au la angeweza niambia personally, nikahojiwa na mimi nikasema siwezi ongea ni mkubwa wangu tena hasa sasa anavyoutafuta ugali wa chama, Mungu awe nawe kwenye wakati huu mgumu"
Steve Nyerere ameshindwa kwenye kura za maoni kwa kupata kura 6 ambapo mshindi ni Jesca Msambatavangu aliyepata kura 190, ambapo jimbo hilo lilikuwa na jumla ya watia nia 57.