Kulia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli, kushoto ni msanii Alikiba
Alikiba amesema Rais John Pombe Magufuli amewaomba watanzania tuweze kudumisha amani kwa sababu yeye amefanya mengi kilichobakia ni sisi kutimiza na usalama utakuepo siku ya mchezo huo.
"Nilimuomba Rais Magufuli aweze kutusaidia kitu kwa hiyo kuna uwezekano wa kuwa na suprise, msije mkashangaa Rais akaja kwa sababu yeye ni mpenzi wa burudani na anatukubali wote mimi pamoja na Samatta, Pia amempongeza sana Mbwana Samatta tulivyokuwa Dodoma kwa kazi kazi nzuri, hivyo tunasubiria suprise yake na chochote kinaweza kutokea kwenye siku ya mchezo huo" amesema Alikiba
Zaidi tazama kwenye video hapa chini.