Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mafuta mengine kugunduliwa Mto Manonga

Thursday , 10th Sep , 2020

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), limeanza hatua ya awali ya utekelezaji wa mradi wa utafutaji wa mafuta katika bonde la Mto Manonga, baada ya utafiti wa awali kubaini uwepo wa miamba yenye viashiria vya mafuta katika bonde la mto huo.

Mitambo ya TPDC

Mradi huo ujulikanao kama Eyasi-Wembele unatatekelezwa katika Mikoa ambayo Mto huo unapitia ikiwemo Bonde la Ziwa Eyasi na Bonde la Mto Manonga unaopatikana katika Mikoa ya Tabora, Shinyanga, Singida na Manyara.

Akitambulisha Mradi huo kwa uongozi wa Mkoa wa Shinyanga, Mtaalam Mshauri wa Mradi huo Dkt Allan Mzengi kutoka TPDC, amesema kuwa mradi huo unaanza na hatua ya awali ya kuangalia athari za kimazingira katika Wilaya Kishapu Mkoani Shinyanga hatua itakayoshirikisha wadau kuanzia ngazi ya Mkoa hadi Kata.

Dkt Mzengi ameongeza kuwa licha ya kuangazia suala la kimazingira, hatua ya pili ya mradi huo itakuwa ni ujenzi wa Mkuza katika eneo ambalo mradi huo utatekelezwa na baadaye kuweka vilipuzi vitakavyosaidia kubaini maeneo ya ujenzi wa visima vya majaribio ya utafutaji mafuta katika eneo la mradi.

Kwa upande wake Mjiolojia kutoka TPDC Gaston Canuty, amesema kuwa tayari TPDC imeishachimba visima vifupi katika eneo la mradi ili kubaini miamba yenye uwezekano wa kuhifadhi mafuta na sasa mradi huo unakusudia kwenda mbali zaidi, kuangalia mafuta yako wapi chini ya ardhi baada ya kubaini miamba hiyo katika eneo la Kishapu.

Utafiti wa Mafuta katika eneo la mradi ulianza kwa kutumia Ndege ya utafiti ambayo iliwawezesha kuona maeneo yenye miamba yenye tabaka gumu na ile ya tabaka laini na kwa kanuni za kijiolojioa maeneo yale ambayo yana mkandamizo mkubwa wa miamba ndiyo yatakayofanyiwa jaribio la utafutaji mafuta. 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala