
Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo
DC Jokate amesema hayo alipotembelea kituo cha mafunzo ya Mbwa na Farasi kinachosimamiwa na jeshi la polisi ikiwa ni ziara yake ya kujionea namna wanyama hao wanavyoweza kutumika katika kukabiliana na matukio ya uhalifu.
Aidha Jokate ameongeza kuwa nia ya serikali ni kuona Taifa linakuwa na utulivu wakati wote, hivyo akaiasa jamii za wakulima na wafugaji kujiepusha na migogoro ambayo imekua ikihatarisha uvunjifu wa amani kila uchwao.