
Kiungo wa Bayern Munich, Joshua Kimmich (wapili kutoka kulia)akitolewa uwanjani baada ya kuumia katika mechi dhidi ya Borussia Dortmund
Raia huyo wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 25, aliondolewa dimbani dakika ya 36 baada ya kujaribu kumzuia Erling Haaland na kwa bahati mbaya alijikuta akipata jeraha.
Taarifa rasmi kutoka klabuni hapo zimeongeza kwamba upasuaji wa goti la Kimmich umefanyika kwa mafanikio na atakosa mechi za timu yake ya Taifa dhidi ya Ukraine, Hispania na Jamhuri ya Czech.
Kimmich amekuwa msaada mkubwa kwa Bayern tangu kuondoka kwa Thiago Alvantara aliyetimkia katika klabu ya Liverpool nchini Uingereza .