Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

WanaCHADEMA waja na hili kuhusu Mdee na wenzake

Thursday , 26th Nov , 2020

Aliyekuwa mtia nia wa Urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA), Leonard Manyama ameelezea mtazamo wake juu ya wabunge 19 walioapishwa jijini Dodoma wa chama hicho bila idhini ya chama kuwa ni usaliti.

Aliyekuwa mtia nia Urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA), Leonard Manyama

Akizungumza katika kipindi cha Supa breakfast, cha East Africa Radio, Manyama amesema ni matarajio yake kuwa wabunge hao watashikilia msimamo wao kuwa ni wabunge halali ilihali hawajatumwa na chama wala kanuni na miongozi ya chama kuzingatiwa.

“Kinachotokea kinataka kukatisha watu tamaa hakina hatma nzuri kwa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, kilichofanyika ni usaliti kwa chama nadhani katibu anapaswa akatazama kwa maslahi mapana ya chama, wanachama na taifa kwa ujumla "amesema Manyama

Aidha kufuatia hayo yaliyojiri Manyama amewashauri viongozi wa chama chake kuchukua hatua juu ya wabunge hao kwani wengi wao wana nyadhifa mbalimbali ndani ya chama kitaifa.

“Kitu kinachotakiwa kifanyike ukiangali wengine ni viongozi wa chama kitaifa, wajumbe kwa maslahi ya nchi, chama, na taifa kiujumla  ningeshauri viongozi wa chama wawaache waendelee na hicho walichokiona kinafaa lakini wanaweza kuwavua nyadhifa zao zote kwenye chama, ili kujenga uaminifu kwenye chama” amesema Manyama

Kwa upande wake Dkt. Mayrose Majinge ambaye pia alikuwa mtia nia wa nafasi ya urais katika chama hicho amesema kuwa hawezi kusema lolote kuhusiana na suala hilo  mpaka awe amejiridhisha kwa kuwa na maelezo na data za kutosha huku akiamini ni mapema mno kuzungumza suala liliotokea.

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi