Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TFF yakemea vikali kauli za ubaguzi kwenye soka

Thursday , 3rd Dec , 2020

Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) limekemea kauli zenye lengo la kuzuia haki ya mashabiki kuingia viwanjani.

Taarifa hiyo ya TFF imesainiwa na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Cliford Mario Ndimbo

Taarifa iliyotolewa na kusainiwa na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Cliford Mario Ndimbo inasema,

“Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) linakemea kwa nguvu kauli zenye lengo la kuzuia haki ya washabiki kuingia viwanjani.”

Taarifa hiyo ikasisitiza kuwa, “kwa mujibu wa katiba ya shirikisho la kimataifa la mpira wa miguu FIFA na ile ya TFF, vitendo vya aina yoyote ya ubaguzi havikubaliki katika mpira wa miguu. Hivyo mshabiki yeyote anaruhusiwa kuingia kwenye mechi ya mpira wa miguu nchini ikiwa tu havunji sheria na taratibu za mpira wa miguu ambazo zimeainishwa kupitia katiba na kanuni husika''.

Taarifa hiyo ilimaliza kwa kusema, ''Hata klabu ambazo zinamiliki viwanja, hutenga tiketi maalum kwa ajili ya timu pinzani na makundi maalum.”

Taarifa hii ya TFF imekuja baada ya hapo jana Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba Haji Manara, kusema kuwa mchezo wao wa kimataifa wa klabu bingwa Afrika wa hatua ya awali wa mkondo wa pili dhidi ya Plateau United ya Nigeria, kuwa mashabiki wa klabu hiyo pekee ndio wanapaswa kuingia uwanjani kwenye mchezo huo na mashabiki wa timu nyingine tofauti na Simba SC wasijitokeze kwenye mchezo huo.

Kauli ya Manara imezua mijadala miongoni mwa mashabiki na wadau wa soka wakiamini kauli hiyo inaweza, kusababisha migogoro au vurugu miongoni mwa mashabiki endapo kama mashaki tofauti na wale wa klabu ya Simba watajitokeza katika mchezo huo.

HABARI ZAIDI

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma