Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Namibia na Tanzania zaweka rekodi makundi CHAN

Wednesday , 20th Jan , 2021

Kundi la timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kundi D, kwenye michuano ya CHAN, limeweka rekodi ya kuwa na mabao mengi kuliko makundi yote tangu kuanza kwa michuano hiyo, inayoendela nchini Cameroon, kundi hilo limezalisha jumla ya mabao 5 kwenye michezo 2.

kiungo wa timu ya Taifa ya Zambia Collins Sikombe akiifungia zambia bao la kwanza kwa mkwaju wa penati kwenye ushindi wa bao 2-0 dhidi ya timu ya taifa ya Tanzania Taifa stars

Taifa Stars ndio ilikuwa timu ya kwanza kuruhusu mabao mawili kwenye fainali za CHAN kwa kufungwa na Zambia mabao 2-0, kwenye mchezo wa kundi D, na tukashuhudia ushindi mkubwa wa kwanza kwenye michuano hiyo, kwenye mchezo mwingine wa kundi hilo ambapo Guinea waliifunga Namibia mabao 3-0.

Sasa kundi hilo ndilo lililozalisha mabao mengi zaidi kuliko makundi yote kwenye fainali hizo likiwa limezalisha mabao 5, wakati kundi linalofuata kuwa na mabao mengi ni kundi A, ambalo limezalisha mabao 2, katika michezo yake 2 ya awali ambapo wenyeji Cameroon walishinda bao 1-0 dhidi ya Zimbabwe, na Mali wakaifunga Burkina Faso 1-0.

Kundi B na C yote yamezalisha bao moja moja, kwenye kundi B michezo yake ya kwanza ilizalisha bao 1 tu ambapo DR Congo waliifunga Congo Brazavill 1-0, na mchezo mwingine wa kundi hilo kati ya Libya na Niger ulimalizika kwa suluhu. Bao la pekee kwa kundi C lilifunga na timu ya taifa ya Morocco kwenye ushindi walioupata wa 1-0 dhidi ya Togo, na Rwanda na Uganda wakatoshana nguvu kwa mchezo wao kumalizika kwa suluhu.

Mpaka sasa yamefungwa jumla ya mabao 9 kwenye mashindano haya huku mabao 5 yakiwa yametoka kwenye kundi D, na kwa ujumla mashindano haya yana wastani wa bao 1.13 kufungwa kwa kila mchezo kwenye michezo 8 iliyochezwa mpaka sasa.

Fainali hizo zitaendelea tena leo kwa michezo miwili ya kundi A, wenyeji Cameroon watacheza dhidi ya Mali mchezo utakaochezwa Saa 1:00 Usiku na Burkina Faso wataminyana na Zimbabwe Saa 4:00 Usiku.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa