Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bayern yatinga fainali kombe la Dunia la vilabu

Tuesday , 9th Feb , 2021

Mabingwa wa bara la Ulaya, klabu ya Bayern Munich ya nchini Ujerumani imetinga hatua ya fainali ya michuano ya kombe la Dunia la vilabu baada ya usiku wa jana wa Februari 9, 2021 kuwafunga mabingwa wa bara la Afrika, klabu ya Al Ahly mabao 2-0 kwenye dimba la Al Rayyan nchini Qatar. 

Wachezaji wa Bayern wakishangilia baada ya kupata bao la kwanza usiku wa jana.

Mabao ya ushindi ya mchezo huo, yote yamefungwa na mchezaji bora wa Dunia wa FIFA wa mwaka 2020, Robert Lewandowski aliyefunga bao la kwanza dakika ya 17 na la pili dakika ya 85 na kuwakatisha matumaini ya kuiona fainali mabingwa hao wa kihistoria barani Afrika.

Mabao hayo yanamfanya mshambuliaji huyo hatari Duniani kwasasa, kufikisha mabao 29 na kutengeneza mabao mengine 7 katika michezo 27 aliyoichezea klabu yake ya Bayern Munich kwenye michuano yote tokea kuanza kwa msimu huu.

Ushindi huo unaifanya Al Ahly kupoteza nusu fainali yake ya tatu na kumruhusu Bayern Munich kutinga fainali hiyo kwa mara ya pili ndani ya miaka takribani saba baada ya mara ya mwisho kutwaa kombe hilo mwaka 2014 baada ya kuwa mabingwa klabu bingwa Ulaya mwaka 2013.

Bayern watacheza fainali hiyo na mabingwa wa bara la Amerika ya kaskazini, Tigres UANL ya nchini Mexico ambaye imetinga hatua hiyo kwa mara ya kwanza baada ya kuwatoa wababe wa nchini Brazil, klabu ya Palmeira kwa kuwafunga bao 1-0.

Mchezo wa fainali ya kombe la Dunia la vilabu utachezwa siku ya Alhamisi ya tarehe 11 Februari 2021, pamoja na mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu wa michuano hiyo ambapo Al Ahly ya Misri  atachuana na Palmeira ya Brazil.

Kama Bayern wakifanikiwa kubeba kombe hilo, basi watafikia rekodi ya mwaka 2008-09 ya FC Barcelona ya Hispania ya kutwaa mataji yote makubwa kwenye ngazi ya vilabu ndani ya msimu wao wa mafanikio baada ya Bayern kutwaa Bundesliga, DFB Pokal, klabu bingwa Ulaya na hata la Uefa Super Cup.

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi