Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Meridian Bet yamsaidia mchimbaji aliyepata ulemavu

Tuesday , 9th Feb , 2021

Kampuni ya michezo ya kubashiri Tanzania MERIDIAN BET imejitokeza kumsaidia Kijana Shabani Salum (34) Mkazi wa Chanika Jijini Dar es salaam aliyekuwa mchibaji wa madini baada kupata ugonjwa ambao bado haujajulikana hali iliyosababisha kulala kitandani kwa zaidi ya miaka 10.

Pichani Kijana Shabani Salum (34) Mkazi wa Chanika Jijini Dar es salaam aliyekuwa mchibaji wa madini baada kupata ugonjwa ambao bado haujajulikana.

Awali akielezea chanzo cha tatizo hilo Shabani anasema alianza kupata maumivu ya bega akaenda hospitali akiwa mzima aliporudi akapanda kitandani kwa ajili ya kupumzika tangu siku hiyo hajawai kuinuka tena ikiwa ni miaka 10 mpaka sasa.

"Siku moja nikiwa nyumbani nilisikia maumivu ya bega nikaenda hospitali kwa ajili ya kupata dawa ya kuchua nikapewa, niliporudi nyumbani nikawa na uchovu nikaingia chumbani kupumzika nilipolala sikuweza kuinuka tena tangu mwaka 2011 hadi leo badala yake miguu ikaanza kujikunja na kuwa midogo sana huku ikiuma mno, napata maumivu makali sana usiku silali tumbo linajaa maji" amesema

Akizungumza wakati akitoa msaada wa Vyakula na Fedha Kiasi cha Shilingi laki sita (600000) Meneja Ustawi Kampuni ya Meridian Bet, Amani Maeda amesema kampuni hiyo imekuwa ikitoa msaada kwa jamii zenye uhitaji mara kwa mara na hivyo wakaguswa na matatizo anayoyapitia Shabani na familia yake kwa sasa sambamba na kuahidi kuendelea kuisaidia familia hiyo zaidi.

"kampuni yetu imekuwa ikisaidia jamii zenye uhitaji mara kwa mara kama sehemu ya kurudisha kwa jamii kwa namna inavyotuunga mkono na kiukweli tumeguswa sana na matatizo anayoyapitia kijana huyu na familia yake hivyo tumewaletea vyakula na fedha shilingi 600000 na tutaendelea kushirikiana nao kwa ukaribu zaidi." amesema

Kwa upande wake Shabani Salum ameishukuru Kampuni ya Meridian Bet kwa msaada huo kwani utasaidia katika maisha yao ya kila siku yeye pamoja na familia yake

Nao Wazazi wa Shabani mbali ya kuishukuru Kampuni hiyo wamesema fedha hizo zitawasaidia kuwaendeleza kiuchumi kwani awali walikuwa na biashara ya sabuni lakini ilikufa kutokana na mtaji kutumika kumuuguzia kijana wao aliyeugua kwa muda mrefu.

Kampuni ya michezo ya kubashiri Tanzania MERIDIAN BET imetoa Unga wa Ugali, Unga wa Ngano, Sabuni ya Unga, Sukari, Mchele, na Mafuta ya kupikia pamoja na fedha kiasi cha shilingi laki sita.

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi