Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wajumbe wa Seneti wa Ufaransa waipongeza Tanzania

Sunday , 21st Feb , 2021

Wajumbe wa Bunge la juu la Ufaransa (SENATE) limeipongeza Tanzania kwa kuwa kinara wa masuala ya utulivu,amani,ulinzi na usalama katika eneo la maziwa makuu hususani katika maeneo ya Mashariki ya Kongo pamoja na eneo la kaskazini mwa Msumbiji.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi

Wajumbe hao ambao pia ni kundi la wabunge marafiki wa Tanzania wametoa pongezi hizo wakati Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi alipotembelea bunge hilo na kuongeza kuwa kupitia Jumuiya za kikanda ikiwemo SADC Tanzania imekuwa kiongozi katika kuhakikisha amani kaskazini mwa Msumbuji na kwamba wajumbe hao wako tayari kuunga mkono jitihada hizo

Katika jitihada za maendeleo zinazofanywa na Tanzania wajumbe hao wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa jitihada zake za kujenga uchumi imara nakusema kuwa wako tayari kuhamasisha watalii wengi kutoka Ufaransa na Ulaya kwenda Tanzania ili kuifanya sekta hiyo kuwa na mchango mkubwa katika uchumi wa Tanzania.

Katika hatua nyingine Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi amezungumza na uongozi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa ambalo limeonesha utayari wa kushirikiana na Tanzania katika masuala ya maendeleo vijijini .

“Katika mazungumzo yetu ya leo tumeangalia maeneo mbalimbali ambayo wapo tayari kushirikiana na Tanzania ambayo ni maendeleo vijijini kwa maana ya umeme, barabra na maji vijijini  lakini pia wameonyesha utayari wakushirikiana na Tanzania katika kutoa mikopo na misaada katika kuimarisha na kukuza uchumi wa bluu” amesema Prof.Kabudi 

Prof Kabudi yupo Paris Nchini Ufaransa kwa ziara ya siku nne kutokana na mwaliko wa Waziri wa Ulaya na mambo ya Nje wa Ufaransa ambapo pia anaitumia fursa hiyo kukutana na makundi ya wafanyabiashara pamoja na taasisi za serikali na binafsi za ufaransa kuhamasisha masuala ya uwekezaji na biashara nchini Tanzania.

 

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi